BAADA ya wasanii waliotoka kwenye mashindano ya u-miss kuvuma sana na
kupotea ghafla, msanii mkongwe kunako gemu la filamu Bongo, Salome
Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ amefunguka na kudai utabiri wake umetimia.
Akizungumza na mwandishi wetu hivi karibuni, Thea alisema miaka kadhaa iliyopita
alitabiri kuwa wasanii waliokuwa wanavuma sana ambao walitokea kwenye
mashindano ya u-miss, hawatadumu kwenye uigizaji hivyo utabiri wake
umetimia kwani sasa hivi, hawavumi tena.
“Utabiri wangu unafanya kazi kwa sababu kwa sasa wale wasanii walioibukia kwenye mashindano ya
u-miss wengi hawasikiki tena, wasanii wanatakiwa kutambua kuwa sanaa hii
siyo lelemama yaani mpaka kufikia hapa tulipo tulifanya kazi ya ziada,
tulisota sana kwenye vikundi,” alisema Thea
No comments:
Post a Comment